Mimi nimezaliwa na kukulia uswazi wakati waifu wangu ni wa kishua.
Jamii niliyokulia (hukoo uswazi kwetu) kuna katabia ka kuwapa watoto majina
kulingana na matukio maarufu yanayotokea au majina ya watu maarufu.
Mfano kuna watoto wanaitwa cossovo, sunami, osama, michael jackson
(kipindi alivokufa), obama, samunge, neymar, baloteli nk....
Kasheshe inakuja kwamba mke wangu amejifungua kidume sasa mimi
nimependekeza tumwite "UKAWA" (kwasababu ndio jina lililobamba kwa sasa
Tz) lakini wife haelewi wala hasikii.
Ubaya au uzuri jina hili limekubalika sana kwa ndugu na marafiki zangu.
Sasa wadau hapo ndipo ninapovurugwa maana mwenyewe nilikua naomba
sana mwanetu azaliwe kukiwa na tukio kubwa ili na mimi niadopt vizuri
utamaduni wetu.
0 comments:
Post a Comment