Facebook
Twitter

SOMA HADITHI KALI NA YA KUSISIMUA "SIMU YA AJABU "

SOMA HADITHI KALI NA YA KUSISIMUA "SIMU YA AJABU "
Fuatilia kisa hiki kila siku jioni kupitia ukurasa wa Simu ya Ajabu. Nawe waweza kutumiwa kisa hiki cha kusisimua kinachosomwa na wengi kupitia whatsapp namba 0713317171 au kuipiga namba hiyo

Thursday, August 7, 2014




Zilikuwa zimepita wiki kadhaa tangu kibanda changu kiwake moto na kuumaliza mtaji wangu kabisa.Na si wajua tena masuala ya hapa mjini d’slamu lazima uanze kutafuta ndugu wa kukusitiri la sivyo utaumbuka.

Nikaenda kwa kaka yangu mmoja ambaye akanipa kazi ya kuchimba shimo la choo pale kwake kwani alihitaji choo cha nje. 

Nikaingia kazini na kupiga kazi kwa moyo wote na siku ya pili shimo likiwa linazidi kushuka chini na sikuwa nasikia kinachoendelea mpaka niliposhtuliwa na kelele za nyumba ile, walikwa wakimpokea ndugu yao aliyekuwa akisoma unesi katika chuo kimoja cha watoto wa kike tuu huko mkoani. 

Nami nikautumia muda ule kutoka mle shimoni na a kupata chakula huku nikimkodolea amimacho ya kufa mtu mtotoyule ambaye alileta raha sana kila ukimtizama.

Siku iliyofuata nikaja na sasa kazi ilikuwa naenda kuimaliza siku hiyo, nikiwa nimekazana kutoa mchanga mle shimoni nikasikia sauti ikiniita ile kukaza macho kumbe yule binti mgeni alikuwa akiniita kwa ajili ya chakula na mbaya zaidi kakaa shimoni pale na baada ya kumchungulia nikagundua hajavaa kufuli……. Mmmh majanga yakaanza hapo.

Kumbe ananitega live akaniambia umependa ulichokiona?nikamjibu ndio akasema kesho nitabaki alone wewe uje muda wowote maana si leo wamaliza kazi???? Nikamwambia poa poa!!!

Kwa uzuri wa yule binti nikawa naona siku ya pili haisogei kabisa yaani, mara siku ya pili ikawadia nikaondoka zangu na kwenda kwenye ahadi. 

Kufika pale nikafunguliwa mlango na kuingia na kweli kama alivyoniambia jana yake kila mtu alikuwa kwenye mishughuliko na watoto wakiwa shuleni kama kawa na kurudi ni kuanzia saa kumi na moja so maisha yalikuwa rahisi sana pale.

Nikaingia na kukaa chumbani na nikaletewa chakula pale kwa raha zangu nikaanza kula huku nikimsubiri aje mamaa alikuwa kanivalia kanga moko.

Akawa anakuja pale tunafanya yetu kisha anaendela na kazi za pale ndani, anakuja tena na mambo yanazidi kusonga na wakati huo mzee nina chupa yangu ya wine pale naishusha taratibuu kama baba wa nyumba vile.

Nikamuuliza, vipi maana wasije rudi? Akaniambia kurudi pale ni kuanzia saa kumi na moja mpaka wawpitie watoto na watoke kazini sio rahisi kuwahi.

Nusu saa baadae mzee akarudi kwa kushtukiza, mtoto akasema atakuwa kuna kitu kasahau hivyo nikae mle chumbani bila kutoa asauti. 

Mzee akaingia ndani mwake kisha akakaa pale sebuleni na akaanza kuongea na simu, “Mama Hellen utawapitia watoto mimi siwezi kwenda leo nipo nyimbani nimewahi toka kazini najisikia uchovu”

Duuuuuuh nikaanza kuhisi mambo yanataka kuharibika pale,kwani siwezi toka mle chumbani mpaka nipite pale sebuleni na madirisha yale hata uso haupenyi.

Sikuwa na jinsi akanibidi nianze kumsikiliza binti yule kwani dalili za yule mzee kuondoka zilianza kuonyesha inafifia.

Mara ikafika saa kumi na moja watoto wakarudi, mimi nimejibanza katika chumba cha dada yule nikiwa kimyatena ile zaidi ya kimya na tayari nilishaanza kujuta uamuzi wangu wa kwenda pale.

Dakika chache baadae binti akaja fasta chumbani na kuniambia niingie uvunguni mwa kitanda kwani dada yake mmoja amabaye anafanya kazi town anarudi hivyo nitulie maana naweza haribu mambo.

Mzee nikaanza kuona nakuwa mfungwa wa matamanio yangu na kama nikishikwa pale hata helayangu ya kuchumba lile shimo nisahau na aibu itakayofuata sio ya kawaida.

Yule dada akaingia nikiwa pale chini akabadili nguo na kisha akaenda kuoga mie hapo namchungulia kiupande na hata hamu ile imekata kata kata, akarudi akajpaka mafuta namuona na kisha kaenda kungana na wenzake kwa ajili ya chakula cha jioni.

Yule binit kaja na kuniambia niwe mpole kwani wakilatu na dada huwahi kulala nitakutoa nje...... Dada akarudi sebuleni kakaaa kafikiri weee kaona itakuwa noma kamwita dada na kumwambia ukweli.

Yule dada bila kujua ameambiwa kaja kaongesa sauti ya mziki mle chumbani kisha kwa sauti akaema, " wewe uliyekuwa ukinichungulia wakati nabadili nguo na kujipaka mafuta hebu toka chini ya kitandsa"

Nilitoka mle uvunguni nikiwa kama nimemwagiwa maji ya baridi.Kisha akaniacha pale na kwenda nje aliporudi akawa kashika chakula akaniambia haya kulamaana nakisikia upo hapa tangu asubuhi, nikamjibu ni sawa nisamehe na nimeshiba chakula,kabla sijamalizia akaniambia unasemaje??????

Nikamdaka na kuchukua chakula nikala huku jasho lanitoka na sijui cha kufanya, majira ya saa saba baada ya wote kulala ndio nikatolewa na yule dada na kufanikiwa kuondoka. Ikanibidi nifikie nyumba ya kulalawageni angalau nipumzike ili asubuhi nianze kufikiri kurudi nyumbani

0 comments:

Post a Comment


  • Copyright 2014 Uvunguni