Facebook
Twitter

SOMA HADITHI KALI NA YA KUSISIMUA "SIMU YA AJABU "

SOMA HADITHI KALI NA YA KUSISIMUA "SIMU YA AJABU "
Fuatilia kisa hiki kila siku jioni kupitia ukurasa wa Simu ya Ajabu. Nawe waweza kutumiwa kisa hiki cha kusisimua kinachosomwa na wengi kupitia whatsapp namba 0713317171 au kuipiga namba hiyo

Wednesday, September 17, 2014

Ona simu hii inavyohangaisha watu





" Mjukuu yaani wewe unaishi kama kipindi mimi niko huko Uruguay nasomea Swimming yaani nilikuwa nakula vitu kama hivi baada ya kupiga vyombo vya kutosha jana yake... 

Vipi mbona ulinifungia? Halafu nimefikaje hapa? maana mara ya mwisho nakumbuka nilikuwa nakula vyombo vyangu sehemu nikiwa na watoto wa mjini.... eeeh haya nieleze umetoka wapi? aliongea bibi huku akinyanyua paja la kuku na kuliweka mdomoni. 

Nesi mwalikumba alishangaa kwa muda na kisha akamuuliza, 

" Hivi wewe ni bibi wa namna gani? kwanza umeniletea matatizo na pili umenifanyia mambo ambayo kamwe sitakuja kuyasahau na sijui yataishaje maana nimechangayikiwa.

Na kama haitoshi huyu aliyeniambia nikutafute ni nani? Tafadhali hebu nifungue maana hadi sasa sielewi na inaonesha ananifahamu vizuri na hiyo dawa uliyoniambia unaniletea iko wapi?" Alihoji nesi mwalikumba huku akionesha dalili za kuchoshwa na bibi gusa unate.

"Ha ha ha ha ha ha ha ha ha ha ha mjukuu wangu, hii ni dunia mi mwenye hapa nilipo ni most wanted yaani usinione niko hivi na muda wote niko vyombo nipo kwenye shuruba ndefu sana. 

Unamfahamu vizuri chamdoli wewe? Unabahati sana maana muda huu wewe nyota yako ingekuwa ilishafifia" aliongea bibi huku akimalizia pegi ya mwisho ya supu yake kwenye sufuria.

Niambie maana simwelewi kabisa na sijui anataka nini katika maisha yangu yaani naomba Mungu mambo haya yasijekufika kazini mbona nitakufa? aliongea mwalikumba


Soma zaidi kwa kubofya hapa

0 comments:

Post a Comment


  • Copyright 2014 Uvunguni