Facebook
Twitter

SOMA HADITHI KALI NA YA KUSISIMUA "SIMU YA AJABU "

SOMA HADITHI KALI NA YA KUSISIMUA "SIMU YA AJABU "
Fuatilia kisa hiki kila siku jioni kupitia ukurasa wa Simu ya Ajabu. Nawe waweza kutumiwa kisa hiki cha kusisimua kinachosomwa na wengi kupitia whatsapp namba 0713317171 au kuipiga namba hiyo

Monday, September 1, 2014

MB DOG AFUNGUKA KUHUSU NANCY SUMARI!

AMERUDI TIP TOP?
Nakukubali sana MB Dog, je, ni kweli umerudi kwenye kundi lako ulilolihama la Tip Top? Juma Kauga, Mwanza, 0655160467
MB DOG: Ni kweli niko nao kwa ajili ya kusimamia kazi zangu maana ndiyo niliyoanza nao.
Msanii wa kitambo katika fani ya Bongo Fleva, MB Dog akipozi.GPL (P.T)
CHANGAMOTO
MB Dog katika maisha yako ya nyumbani hupendi vitu gani ukifanyiwa na watu wasiokutakia mambo mema katika mafanikio yako kuhusiana na muziki wako? Je, unakutana na changamoto za aina gani wewe ukiwa kama kioo cha jamii hapa Bongo? Salim Liundi, Dar, 0659601205
MB DOG: Changamoto ni nyingi sana, mimi sina dharau na huwa sipendi kabisa dharau hivyo mtu anaponidharau huwa inaniuma sana ila nikimpatia nafasi nampa vidonge vyake sawasawa.
UKIMYA
MB Dog mbona kimya sana kwenye gemu au mipango hovyo? Tuambizane nasi tujue kaka. Nick Kanje, Moro, 0654108014
MB DOG: Mipango bado inaendelea na hivi karibuni mtasikia kazi zangu mpya nyingi tu.

SWALI
Ulianza lini muziki na nani alikuvutia mpaka ukaamua kufanya muziki? Je, nani huwa unamkubali kwenye Bongo Fleva kwa sasa? Loth Chigonela, Moro, 0788133987
MB DOG: Muziki nilianza mwaka 1995 lakini nilikuja kuchomoka mwaka 2002. Nilikuwa navutiwa sana na wanamuziki wanaochana yaani Hip Hop akina (Juma) Nature lakini baada ya kuingia kwenye gemu nikajikuta kwenye Bongo Fleva. Kuhusu ninayemkubali mimi naona wote wanafanya vizuri tu.
TIP TOP CONNECTION 
Unafikiri usingerudishwa mjengoni na Tip Top Connection ungeweza kusimama wewe kama wewe na ukaeleweka kwa mashabiki wako? Nyandonge Deusy, Shinyanga, 0766438657
MB DOG: Naamini Mungu ndiye mpangaji wa kila jambo hivyo yeye angejua ningesimama vipi.
YEYE NA NANCY SUMARI
MB Dog hivi ni kweli ulikuwa na uhusiano wa kimapenzi na Nancy Sumari? Msomaji, 0652672805
MB DOGO: Hapana nilikuwa shabiki wake tu.
KUBANA PUA
Hivi kwa nini msanii ni mtu tofauti na jamii nyingine, mnapenda kujipa maisha ambayo hamna, kwa nini mnapenda kubana pua? Ramadhan Mbogo, 0656380201
MB DOG: Wapo wanaobana pua na kuishi maisha feki lakini mimi naishi maisha ya kawaida sana.
KOLABO NA DIAMOND
Nakukubali sana kwa sauti yako na mashairi yako, je, bado hujafikiria kufanya kazi na Diamond Platnumz? Kadabla, Dar, 0714668505
MB DOG: Nina mpango wa kufanya naye kolabo lakini ni baada ya kutoa kazi nyingi zangu mwenyewe.
HUYU ANAHOJI
Mdogo wangu MB Dog kwa nini ndoa zenu mnaojiita mastaa wa Bongo hazidumu? John Ipembe, Shinyanga, 0759918465
MB DOG: Sidhani. Hiyo ni dhana tu na inatokea kwa baadhi na siyo wote.
KOLABO
Kiukweli kati ya wasanii ninaowakubali mmojawapo ni wewe, naomba kama hutajali unishirikishe kwenye video yako yoyote utakayotoa. Ramasingo, Dar, 0717674336
MB DOG: Haina tabu kikubwa tuwasiliane tu.
MAFANIKIO
Napenda kujua MB Dog tangu uanze muziki ni mafanikio gani umeyapata? Moshi, Dar, 0762981249
MB DOG: Mafanikio ni mengi lakini kubwa zaidi nimeweza kufahamika sehemu kubwa ya ulimwengu pia najitegemea na ninategemewa.
KUOA
Kiukweli muziki wako unanivutia sana. Pia una mafundisho ya kiukweli hongera, wasanii wengi wanadai kuoa ni kushuka kimuziki na wewe umeoa. Je, hili kwako unalionaje? Msomaji, 0755203757
MB DOG: Siyo kweli, hizo ni hisia tu mbona kuna wanamuziki wameoa na wanaendelea kufanya vizuri.
HUYU ANATAKA KUJUA
MB Dog mimi nakujua ulikuwa na ukaribu sana na Maryam Mzulu ila nataka kujua uhusiano wenu na ukaribu kwa jumla. Kareem Smart, Tanga, 0713044638
MB DOG: Simjui huyo.
KABILA 
Upo juu kaka, napenda sana nyimbo zako. Pia napenda kujua wewe ni kabila gani na una umri gani? Stella Hegga, Dar, 0718632577
MB DOG: Asante, kabila langu ni Msegeti, umri ni siri yangu.
NJE YA FANI
MB Dog, tofauti na sanaa ya muziki unajishughulisha na nini? Mido, Moshi, 0758872458
MB DOG: Biashara.
WIMBO
Naona uko njema ndani ya gemu la Bongo Fleva na mimi ni kati ya mashabiki wako, vipi kuhusu Umenuna ni stori ya kweli au wazo tu? Nico Yohana, Mtwara, 0689785257
MB DOG: Ni wazo tu.
WATOTO
Najua una watoto wawili, mbona uko kimya sana? Msomaji, 0713642299
MB DOG: Kweli nina watoto wawili, ukimya una mwisho wake na kimya kingi kina mshindo, subiri kazi mpya zinakuja nyingi. 

0 comments:

Post a Comment


  • Copyright 2014 Uvunguni