Facebook
Twitter

SOMA HADITHI KALI NA YA KUSISIMUA "SIMU YA AJABU "

SOMA HADITHI KALI NA YA KUSISIMUA "SIMU YA AJABU "
Fuatilia kisa hiki kila siku jioni kupitia ukurasa wa Simu ya Ajabu. Nawe waweza kutumiwa kisa hiki cha kusisimua kinachosomwa na wengi kupitia whatsapp namba 0713317171 au kuipiga namba hiyo

Saturday, August 16, 2014

UKATILI: KIGOGO Amchoma Kisu Mkewe

KIGOGO wa shirika moja la kimataifa linalojishughulisha na watoto yatima, tawi la mkoani Pwani, Tanzania aliyetajwa kwa jina moja la Mugaka, anayekadiriwa kuwa na umri kati ya miaka 35 hadi 40, ametupwa rumande akituhumiwa kumchoma kisu na kumtoa manundu mkewe, Leah (28).
Mke wa kigogo (Mugaka),Bi. Leah aliyefanyiwa unyama na mumewe.
Mke wa kigogo (Mugaka),Bi. Leah aliyefanyiwa unyama na mumewe.
Tukio hilo la kusikitisha lilijiri wilayani Kisarawe, Pwani mwishoni mwa wiki iliyopita. Kwa mujibu wa habari zilizopatikana, chanzo cha unyama huo kinashangaza huku madai ya Mugaka ambaye ni afisa mshauri wa shirika hilo yakisema mkewe huyo amekuwa akimjazia choo kwa kuwa tangu amuoe miaka mitatu iliyopita, ameshindwa kumzalia mtoto.
Sehemu ya mguu alipochomwa kisu na Bw. Mugaka (mumewe).
Sehemu ya mguu alipochomwa kisu na Bw. Mugaka (mumewe).

Habari ziliendelea kudai kwamba shirika analofanyia kazi Mugaka linalosimamiwa na mfuko wa rais wa zamani wa Marekani, Bill Clinton. Madai mazito yalishushwa kwamba Mugaka amekuwa akimnyanyasa mkewe kwa sababu hiyo, kiasi cha kumtolea maneno ya kejeli, dharau, kashfa huku akimshushia kipigo ‘hevi’.
Majeraha mengine sehemu ya mguu wa kulia.
Majeraha mengine sehemu ya mguu wa kulia.

Ilisemekana kwamba ilifika wakati hali ikawa mbaya kiasi cha baadhi ya majirani kumshauri Mugaka kuachana naye kama anaona hamfai. Ilisemekana kwamba chanzo cha kufanyiwa unyama huo na kujeruhiwa na kisu ni madai ya mwanaume huyo kuwa alitumiwa ujumbe mfupi kwenye simu yake, akiambiwa kuwa mkewe alikuwa akimsaliti kwa kutembea na watu wa nje, wakiwemo polisi.
Kigogo anayetajwa kwa jina moja la Mugaka anayetuhumiwa kumnyanyasa mkewe.
Kigogo anayetajwa kwa jina moja la Mugaka anayetuhumiwa kumnyanyasa mkewe.

Ilidaiwa kwamba mkewe alikataa madai hayo na kumtaka mumewe kuitoa namba ya simu iliyotuma ujumbe huo ili wampigie palepale wakiwa wote, lakini jamaa huyo alikataa na kumshambulia sehemu mbalimbali za mwili huku akimchoma na kisu pajani.
Jirani wa mtuhumiwa aliyeomba hifadhi ya jina alidai kwamba Mugaka amekuwa akimpiga, kumtesa, kumdhalilisha mkewe mara kwa mara huku akisikika kumweleza kuwa ipo siku atamuua.
Muonekano wa karibu wa Bi. Leah.
Muonekano wa karibu wa Bi. Leah.

Baba mzazi wa majeruhi, William Lyima alisema baada ya kupata taarifa za kipigo hicho, alimpigia simu Mkuu wa Kituo cha
Polisi cha Kisarawe, OCD Issa na kumtaarifu tukio hilo ambapo askari wake walifika na kuizingira nyumba ya mtuhumiwa huyo na ilipofika majira ya saa 11:00 alfajiri walifanikiwa kumtia mbaroni. Kigogo huyo amefunguliwa mashitaka ya shambulio la kudhuru mwili na
kujeruhi kwa kisu katika jalada lenye kumbukumbu namba KIS/RB/964/2014-SHAMBULIO LA KUDHURU NA KUJERUHI MWILI akisubiri sheria kuchukua mkondo wake.

Credit: GPL

0 comments:

Post a Comment


  • Copyright 2014 Uvunguni