Facebook
Twitter

SOMA HADITHI KALI NA YA KUSISIMUA "SIMU YA AJABU "

SOMA HADITHI KALI NA YA KUSISIMUA "SIMU YA AJABU "
Fuatilia kisa hiki kila siku jioni kupitia ukurasa wa Simu ya Ajabu. Nawe waweza kutumiwa kisa hiki cha kusisimua kinachosomwa na wengi kupitia whatsapp namba 0713317171 au kuipiga namba hiyo

Saturday, August 23, 2014

 
Kundi la la wapiganaji wa Kiislamu la Iraq na Syria (ISIS) limetekeleza mauji ya kutisha kwa kumkata kichwa mwandishi wa habari wa Marekani.

Mwandishi huyo ambaye pia ni mpiga picha mashuhuri aliyetajwa kwa jina la James Wright Foley alikamatwa na wanajeshi wa kundi hilo mwaka 2012 nchini Syria alikokuwa akiripoti habari za kuondolewa madarakani Bashir Al-Assad.
Katika video inayoonesha mauaji hayo iliyowekwa YouTube inamuonesha mtu aliyemkata kichwa mwandishi huyo akiwa amejifunika uso kwa mask akiongea kiingereza kwa lafudhi ya Uingereza, akidai kuwa wanafanya hivyo kama sehemu ya kulipiza kisasi kwa rais Obama aliyetoa amri ya mashambulizi ya anga dhidi ya kundi hilo nchini Iraq.
Msemaji wa ISIS, ameonya kuwa kutakuwa na tukio lingine la kulipiza kisasi kwa kumkata kichwa mwandishi wa Marekani Steven Sotloff wanaemshikilia

0 comments:

Post a Comment


  • Copyright 2014 Uvunguni