Facebook
Twitter

SOMA HADITHI KALI NA YA KUSISIMUA "SIMU YA AJABU "

SOMA HADITHI KALI NA YA KUSISIMUA "SIMU YA AJABU "
Fuatilia kisa hiki kila siku jioni kupitia ukurasa wa Simu ya Ajabu. Nawe waweza kutumiwa kisa hiki cha kusisimua kinachosomwa na wengi kupitia whatsapp namba 0713317171 au kuipiga namba hiyo

Thursday, September 4, 2014

Na Imelda Mtema
STAA wa Mduara, Zuwena Mohamed ‘Shilole’ amefungua kinywa chake na kusema mpenzi wake wa sasa, Nuh Mziwanda ndiye anayemtibu vizuri kunako ‘sita kwa sita’ japokuwa watu wengi wamekuwa wakiudharau mwili wake.

Akizungumza na gazeti hili bila kung’ata maneno, Shilole alisema wengi wanashindwa kujua kwamba mtu anaweza kuwa na mwanaume mwenye umbo kubwa lakini akawa hayajui mapenzi lakini mwenye umbo dogo kama Nuh, akawa ni bingwa wa mapenzi.

Akiendelea kumwaga data mbele ya kinasa sauti cha Amani, msanii huyo anayetamba na wimbo wa Nakomaa na Jiji alisema kuwa katika mapenzi, umri wala ukubwa wa umbo hauna maana yoyote.
“Yaani kwa kweli Nuh ananimudu na tunaenda sawa katika suala zima la mapenzi, kwa hiyo sioni udogo wake kwangu, kwa upande wangu Nuh ni mkubwa sana watu wasiangalie mwili,” alisema Shilole pasipo kutaja umri wa mpenzi wake huyo.

Shilole aliongeza kuwa, kutokana na mahaba ya nguvu anayoyapata kutoka kwa mpenzi wake huyo, anapata nguvu ya kufanya kazi vizuri siku hadi siku hivyo hapati tamaa.
“Sina stress za mapenzi na mara nyingi nafanya kazi zangu zinaenda sawa kabisa,” alimalizia Shilole.
Source-GPL

0 comments:

Post a Comment


  • Copyright 2014 Uvunguni