Facebook
Twitter

SOMA HADITHI KALI NA YA KUSISIMUA "SIMU YA AJABU "

SOMA HADITHI KALI NA YA KUSISIMUA "SIMU YA AJABU "
Fuatilia kisa hiki kila siku jioni kupitia ukurasa wa Simu ya Ajabu. Nawe waweza kutumiwa kisa hiki cha kusisimua kinachosomwa na wengi kupitia whatsapp namba 0713317171 au kuipiga namba hiyo

Thursday, April 2, 2015

1.Usiwe mtu wa kulalamika kwa sababu hakuna mtu liye sahihi sana katika maisha haya.
2. Usimlaumu mtu hapa duniani kwani ulizaliwa peke yako na kila jukumu mbele yako ni lako wewe na utakufa peke yako.
3. Usijaribu kulazimisha watu wafikiri kama wewe au kuwahukumu watu kwa jinsi unavyofikiria wewe, jitahidi kuwa upande wa pili wa wao kabla ya maamuzi
4. Usiwe mtu wa kunung’unika kila wakati kwani hiyo hukupunguzia mori na ari ya kazi
5. Usijimilikishe mambo na majukumu makubwa ukidhani utaishi milele kuwa na kiasi nacho hakitapotea….
6. Usijisifie na kujipa ufahari mapema kumbuka bado tupo safarini na kunaweza kutokea lolote njiani
7. Usiwe na wivu mbaya kwani kila kitu ni matokeo ya mtu kujituma na Mungu kukamilishia mipango yake kwako.
8. Kamwe usitengeneze nafasi ya kisasi katika moyo wako kwani malipo yake huangamiza nafsi na moyo wako pia
9. Usijaribu kwa namna yoyote kumsababisha mtu akakosa riziki yake na familia yake kwa makusudi au bahati mbaya, dhambi hiyo huwa na doa lisilofutika na hukuandama kama laana
10. Kuwa mwepesi wa shukrani kwa kila jambo jema kwako hata kama ni dogo kiasi gani
11. Daima epuka: Unafiki, Umbea na majungu bali wewe kuwe mwenye busara kwa kila jambo
12.Tabasamu na kumtakia rafiki yako siku njema

Dunia imejaa visa na mikasa ambayo kila mtu hukutana nayo kwa nafasi yake. Lakini wakati wewe unafikiri ya kuwa umeumia au kuumizwa zaidi wapo ambao wao wanapitia makubwa zaidi yako.

Kuna watu wao baada ya kupitia mapito haya hukata tamaa ila kuna ambao wao hupigana mpaka tone la mwisho kuhakikisha wanakabiliana na changamoto hizo.


Kuna wale ambao hudhania umaskini ndio sababu kubwa ya kuwafanya wawe makatili hasa wakiangalia wapi walikopitia, lakini pia kuna wale ambao kutokana na mali na utajiri wao huamua kutumia fedha hizo kulipa visasi au hata kuhatarisha maisha ya wenzao.

Kutana na SAMIRA katika simulizi hii na ujifunze mengi.

Hapo chini kuna link za simulizi hii kuanzia namba moja mpaka ilipofikia sasa, na kuanzia leo ukiikosa hapa basi utaikuta kupitia karibumbeya.com


Soma  sehemu ya 8

Soma visa vingine HAPA


1. Huwezi kuwapenda watu wa nje kama huna mapenzi ya dhati kwayule uliyenaye kwenye uhusiano sasa.

2. Kumsaliti mwezio kwa kisingizio cha kulipiza kisasi huwa njia rahisi ya kukuingiza katika mgogoro binafsi na mwishowe kukuharibia kila mipango yako.

3. Kamwe usijidanganye kuwa utaweza kumsaliti na kumdanganya mwenzio kwa muda mrefu bila kugundulika, kila usaliti ni sawa na mimba lazima kuna muda utafika kila mtu ataiona tu.

4. Mahusiano yoyote hujengwa na uaminifu na kuthaminiana huku neno samahani na nimekusamehe likiwa nguzo kwa utatuzi wa kila tatizo mbele yenu.

5. Kusema nisamehe sio kuonekana mjinga bali pia huweza kukupa heshima na kuongeza mapenzi ya dhati baina ya yenu.

6. Neno nitakuacha au tuachane isiwe silaha ya kumwonea mwenzio maana nalo likizoeleka huweza kumfanya mwenza wako kuchukua maamuzi magumu kwani huashiria wewe una watu huko nje wakupao kiburi.

7. Kamwe usiwe mwepesi wa kuamini nini watu wanasema ila mshirikishe mwenzio kila uvumi ukoonyesha kumwamini na kumpa nafasi ya kukupa ufafanuzi.

8. Kila mahusiano huja na Baraka zake na huondoka na Baraka zake, unaweza ona unapata mafanikio sasa kwa sababu ya kuwa na huyo uliyenaye. Hivyo jitahidi kuzitazama kwa makini kila fursa njema upatazo na ona je zikiondoka utakuaje.

9. Fedha huleta ufahari lakini kamwe haina mchango katika kuleta furaha kwenye mahusiano yenu, hivyo pendaneni kama vile ni matajiri na maskini, kwani fedha yaweza kupotea muda wowote na kama mnapendana itarudi pia kwa kushirikishana jinsi ya kuirudisha lakini mapenzi yakiisha hata uwe na gunia la pesa ni kazi bure sawa na kuirudisha ladha ya chumvi siku ikiisha.

10. Mahusiano ya wawili hupendeza kama hayataingiliwa na watu wengine nanyi mkishirikishana katika kutatua matatizo na kuwa na maamuzi ya pamoja kwa kila jambo.

11. Ni vyema kutengeneza mazoea ya kujivunia na kuona ufahari kwa huyo uliyenaye na kama ukishindwa kuyafanya hayo kwa huyu hata ukimpata mpya mchezo utakuwa huo huo kwani bado huna ujuzi wa kuishi na mwenzako.

12. Huitaji kuwa dikteta kwa kuwa na misimamo ya kikoloni bila ya kuwa na utambuzi wa kuwa mko watu wa wili hivyo acha tabia za ubinafsi.

13. Wanawake wazuri na wanaume wenye mvuto hawawezi kwisha amini uliyenaye hukumpata kwa bahati mbaya, mpende kwa dhati.

14. Kila maamuzi ufanyayo sasa ukiwa na stress au huna sress huwa na tabia ya kuihaibu kesho yako, hivyo jitahidi kuwa na subira katika kila jambo.

15. Mapenzi hayaonyeshwi kwa kufungua zipu au kwa binti kupanua miguu tuu, mapenzi ni hisia, jinsi mnavyoishi, maelewano, ushirikiano na mambo mengine mengi.

16. Upendo hausubiri siku ya Valentine, kila siku ifanye kuwa siku ya valentine kwa mpenzi wako.




Posted by Fred Kihwele · 5 hrs · 
Mambo ya muhimu kuzingatia unapokuwa na rafiki katika maisha yako.
1. Usiwe mwepesi wa kutoa lawama na kumhukumu kwa kila jambo ila jaribu kumwelewa na kumfanya akuelewe wewe pia
2. Usijifanye kuwa wewe ni wa muhimu kuliko yeye ila amini yeye ni wa muhimu zaidi jambo litakalo mfundisha nae kukuona wa muhimu

'Mambo ya muhimu kuzingatia unapokuwa na rafiki katika maisha yako.

1. Usiwe mwepesi wa kutoa lawama na kumhukumu kwa kila jambo ila jaribu kumwelewa na kumfanya akuelewe wewe pia

2. Usijifanye kuwa wewe ni wa muhimu kuliko yeye ila amini yeye ni wa muhimu zaidi jambo litakalo mfundisha nae kukuona wa muhimu

3. Kuwa karibu na matatizo yake hata kama huna uwezo onyesha kuwa wewe ni bega lake litakalo mfuta machozi wakati akilia yaani mpe ushauri wenye utatuzi na ajivunie wewe

4. Usiwe mwepesi wa kuropoka kwa watu mapungufu yake ila jitahiti kuwa mwazi kwake na kumbadilisha ikibidi

5. Jaribu kuwa msiri wa kutunza mambo yanayowahusu na kutoyashirikisha kwa wengine

6. Usiwe mwepesi wa kumkatisha tamaa kwa kila jambo.
7. Epuka kuwa mzigo kwa mwenzako nawe jitume na kuonyesha mwenzio anaweza kukutegemea pia

9. Vumilianeni kwa mambo yanayoweza kuwafanya mwonekane kutofautiana na jaribuni kuyamaliza mambo yenu wenyewe.

10. Furahia mafanikio ya mwenzako toka moyoni na chukua kama changamoto za kujifunza nawe ufanye vyema kuliko kuanza kujenga uadui au kumsema vibaya.

11. Jitahidi kuzuia hasira zako zikufanye utoe maamuzi utakayoyajutia baadae.Fanya maamuzi kwa busara katika kila jambo.

12. Jenga tabia ya kuwasiliana na rafiki yako mara kwa mara kama yuko mbali na hata kama mnakaa pamoja

13. Marafiki wema pia huletwa kwa neema ya Mungu hivyo mwombe Mungu marafiki na kumshukuru kwa kuwapata na mwombe akupe hekima na uvumilivu wa kuishi nao
Kitu cha muhimu zaidi ni kwamba kuwa na rafiki mpya kila siku ni rahisi sana. Ila ugumu ni kuweza kubaki na marafiki hao milele.
Hivyo ni vyema kujenga tabia ya kuheshimu uhusiano wa kirafiki na kuilinda

kumbuka kulike @[370489863125466:274:Karibu Mbeya] na tembelea www.karibumbeya.com'

Like ·  ·  · 1143

Posted by Fred Kihwele · 1 hr · 
Kijana asiye na kazi aitwaye Nolesy aliamua kumwoa rafiki yake wa muda mrefu aliyekuwa akifanya kazi katika benki moja mashuhuri.
Nolesy alijitosa katika ndoa licha ya hofu na ushauri mwingi aliopewa na ndugu kuwa ni vibaya kuoa ukiwa huna kazi.
Kila mwezi yule binti alimpa mmewe mshahara wake wote wa 800,000 baada ya kutoa fungu la kumi kwa ajili ya kanisani.
Like ·  ·  · 72

Posted by Fred Kihwele · 3 hrs · 
Dada mmoja alihitimu chuo na kutafuta kazi kwa muda mrefu sana kiasi cha kukaa mika 15 akiwa hana kazi. Mbaya zaidi katika kipindi hicho alipata wakati mgumu namna ya kupata fedha za kujikimu.
Siku moja akawa na elfu tano tu na akaingia katika hoteli moja ili aweze kupata chakula cha mchana, akaketi na kuagiza chakula chake.
Baada ya kuletewa akasali na kabla ya kula chakula wakaingia wazee watatu wakionekana wamechoka na wanajaa pia....
Like ·  ·  · 1791

Posted by Fred Kihwele · 3 hrs · 
Napokea oda za kusambaza fruits salad kwenye maofisi na kwenye sherehe/party



Napokea oda za kusambaza fruits salad kwenye maofisi na kwenye sherehe/party. 0767634082
KARIBUMBEYA.COM


  • Copyright 2014 Uvunguni