1.Usiwe mtu wa kulalamika kwa sababu hakuna mtu liye sahihi sana katika maisha haya.
2. Usimlaumu mtu hapa duniani kwani ulizaliwa peke yako na kila jukumu mbele yako ni lako wewe na utakufa peke yako.
3. Usijaribu kulazimisha watu wafikiri kama wewe au kuwahukumu watu kwa jinsi unavyofikiria wewe, jitahidi kuwa upande wa pili wa wao kabla ya maamuzi
4. Usiwe mtu wa kunung’unika kila wakati kwani hiyo hukupunguzia mori na ari ya kazi
5. Usijimilikishe mambo na majukumu makubwa ukidhani utaishi milele kuwa na kiasi nacho hakitapotea….
6. Usijisifie na kujipa ufahari mapema kumbuka bado tupo safarini na kunaweza kutokea lolote njiani
7. Usiwe na wivu mbaya kwani kila kitu ni matokeo ya mtu kujituma na Mungu kukamilishia mipango yake kwako.
8. Kamwe usitengeneze nafasi ya kisasi katika moyo wako kwani malipo yake huangamiza nafsi na moyo wako pia
9. Usijaribu kwa namna yoyote kumsababisha mtu akakosa riziki yake na familia yake kwa makusudi au bahati mbaya, dhambi hiyo huwa na doa lisilofutika na hukuandama kama laana
10. Kuwa mwepesi wa shukrani kwa kila jambo jema kwako hata kama ni dogo kiasi gani
11. Daima epuka: Unafiki, Umbea na majungu bali wewe kuwe mwenye busara kwa kila jambo
12.Tabasamu na kumtakia rafiki yako siku njema
Dunia imejaa visa na mikasa ambayo kila mtu hukutana nayo kwa nafasi yake. Lakini wakati wewe unafikiri ya kuwa umeumia au kuumizwa zaidi wapo ambao wao wanapitia makubwa zaidi yako.
Kuna watu wao baada ya kupitia mapito haya hukata tamaa ila kuna ambao wao hupigana mpaka tone la mwisho kuhakikisha wanakabiliana na changamoto hizo.
Kuna wale ambao hudhania umaskini ndio sababu kubwa ya kuwafanya wawe makatili hasa wakiangalia wapi walikopitia, lakini pia kuna wale ambao kutokana na mali na utajiri wao huamua kutumia fedha hizo kulipa visasi au hata kuhatarisha maisha ya wenzao.
Kutana na SAMIRA katika simulizi hii na ujifunze mengi.
Hapo chini kuna link za simulizi hii kuanzia namba moja mpaka ilipofikia sasa, na kuanzia leo ukiikosa hapa basi utaikuta kupitia karibumbeya.com
Soma Sehemu ya 2
Soma Sehemu ya 5
Soma Sehemu ya 7
Soma Sehemu ya 9
Soma visa vingine HAPA




!['Mambo ya muhimu kuzingatia unapokuwa na rafiki katika maisha yako.
1. Usiwe mwepesi wa kutoa lawama na kumhukumu kwa kila jambo ila jaribu kumwelewa na kumfanya akuelewe wewe pia
2. Usijifanye kuwa wewe ni wa muhimu kuliko yeye ila amini yeye ni wa muhimu zaidi jambo litakalo mfundisha nae kukuona wa muhimu
3. Kuwa karibu na matatizo yake hata kama huna uwezo onyesha kuwa wewe ni bega lake litakalo mfuta machozi wakati akilia yaani mpe ushauri wenye utatuzi na ajivunie wewe
4. Usiwe mwepesi wa kuropoka kwa watu mapungufu yake ila jitahiti kuwa mwazi kwake na kumbadilisha ikibidi
5. Jaribu kuwa msiri wa kutunza mambo yanayowahusu na kutoyashirikisha kwa wengine
6. Usiwe mwepesi wa kumkatisha tamaa kwa kila jambo.
7. Epuka kuwa mzigo kwa mwenzako nawe jitume na kuonyesha mwenzio anaweza kukutegemea pia
9. Vumilianeni kwa mambo yanayoweza kuwafanya mwonekane kutofautiana na jaribuni kuyamaliza mambo yenu wenyewe.
10. Furahia mafanikio ya mwenzako toka moyoni na chukua kama changamoto za kujifunza nawe ufanye vyema kuliko kuanza kujenga uadui au kumsema vibaya.
11. Jitahidi kuzuia hasira zako zikufanye utoe maamuzi utakayoyajutia baadae.Fanya maamuzi kwa busara katika kila jambo.
12. Jenga tabia ya kuwasiliana na rafiki yako mara kwa mara kama yuko mbali na hata kama mnakaa pamoja
13. Marafiki wema pia huletwa kwa neema ya Mungu hivyo mwombe Mungu marafiki na kumshukuru kwa kuwapata na mwombe akupe hekima na uvumilivu wa kuishi nao
Kitu cha muhimu zaidi ni kwamba kuwa na rafiki mpya kila siku ni rahisi sana. Ila ugumu ni kuweza kubaki na marafiki hao milele.
Hivyo ni vyema kujenga tabia ya kuheshimu uhusiano wa kirafiki na kuilinda
kumbuka kulike @[370489863125466:274:Karibu Mbeya] na tembelea www.karibumbeya.com'](https://fbcdn-sphotos-b-a.akamaihd.net/hphotos-ak-xfp1/v/t1.0-9/s851x315/10981358_422578364583282_4313532731926780394_n.jpg?oh=10b2f8829aaaab27d39ca3a5ed65c41b&oe=558C9803&__gda__=1433665587_86d9731d9c29fe362ae1d3469f6fefe1)

