Facebook
Twitter

SOMA HADITHI KALI NA YA KUSISIMUA "SIMU YA AJABU "

SOMA HADITHI KALI NA YA KUSISIMUA "SIMU YA AJABU "
Fuatilia kisa hiki kila siku jioni kupitia ukurasa wa Simu ya Ajabu. Nawe waweza kutumiwa kisa hiki cha kusisimua kinachosomwa na wengi kupitia whatsapp namba 0713317171 au kuipiga namba hiyo

Monday, August 18, 2014

T.I ashitakiwa kwa wizi wa vifaa vya jukwaani

  T.I ashitakiwa kwa wizi wa vifaa vya jukwaani

Rapper T.I anakabiriwa na kesi ya wizi wa vifaa vya jukwaani ambavyo alivikodi mwaka jana wakati wa Tour ya America’s Most Wanted aliyofaya na Lil Wayne na rappers wengine.
Kwa mujibu waTMZ, kampuni iliyomkodishia vifaa hivyo imeeleza katika shitaka lake kuwa ilimkodishia vifaa T.I na akalipia gharama za kukodisha lakini wakati wa kurudisha hakurudisha Screen ya gharama kubwa  inayofahamika kama Roll Drop inayotumika kuonesha picha na video wakati wa show.
Screen hiyo imetajwa kuwa na thamani ya $50,000 lakini kampuni hiyo inataka T.I ailipe $100,000 kwa kuwa katika muda wote iliyopotea ingekuwa imewaingizia kiasi hicho cha pesa kwa kuwakodishia watu wengine.
Tuhuma hizo zinakuja wakati ambapo T.I anaendelea kupiga kazi ya kuandaa albam yake mpya inayoitwa ‘Paperwork: The Motion Picture.
T.I ameeleza katika mahojiano alioyofanya hivi karibuni kuwa albam hiyo itawashikirisha Rick Ross, The Dream, Lil Boosie, Young Jeezy na wengine wengi.
Bado tarehe rasmi ya kutoka haijapangwa

0 comments:

Post a Comment


  • Copyright 2014 Uvunguni